,

,

,

,
Gossip

Hakuna Beef kati ya Ali Kiba na Diamond ila Kuna Beef kati ya Ali na Sallam

Hii kitu sio mara ya Kwanza kutokea malumbano kati ya Ali na Sallam.

1.Show ya Tigo Dar es salaam

mwaka jana kwenye show ya Tigo ambayo wasanii A List wa bongo flava wote walikuwemo ila baada ya ile show ambayo Ali kama kawaida yake alikimbiza Sallam kesho yake alishinda huko Twitter akimkashifu na kumtukana Ali kuwa ni mchawi na muoga akitoa madai kuwa Ali na timu yake waliruka ukuta kuingia back stage na Ali akumsalimia msanii yoyote kule back stage japo walikuwepo wakina A.Y,Mwana da,Barnaba boy,Ben Pol,Ommy Dimpozi,Diamond na wasanii wengine Kibao.

Hapo ndio utashikwa na mshangao mambo ya Ali kuruka ukuta na kutomsalimia msanii yoyote ikiwa kweli au ni uongo yeye Sallam inamuhusu nini?!
Na mbona wasanii wengine au mameneja wao hawakuzungumzia ile kitu kwanini yeye imuume namna ile na kuropoka kwenye social network kwa kiasi kule??

2.Show ya ODM-Mombasa

Kukawa na Show nyingine Mombasa..Show ambayo haikuwa ya diamond lilikuwa ni Tamasha la Chama cha Siasa ODM cha bwana Raila Odinga na wasanii Kibao wa Mombasa walikuwepo na Diamond alienda pale kama msanii mualikwa.
Kumbuka kuwa Tamasha sio la Diamond ni la Chama cha ODM wenye tamasha Lao wakaamua kumualika na Ali kwa sababu Ali ndio msanii anaekubalika zaidi Kutoka afrika pale Mombasa.

Baada ya lile tamasha Sallam akulala alilalama usiku kucha kwanini hawakuambiwa kuwa Ali angekuwemo kwenye hilo tamasha..basi kama kawaida yake akamtukana Ali kumwita muoga mwenye kusafiria nyota ya Diamond na kusahau kabisa lile tamasha alikuwa la kwao wao bali ni Chama cha Siasa ODM na wote walikuwa waalikwa tu.

3.Coke Studio,Nairobi

Mwaka jana Ali alikuwa Coke studio na kina Neyo kule Kenya na Neyo alikuwa yupo tayari kufanya Solo project na Ali nje ya coke studio..Sallam akulala alifunga safari usiku usiku mpaka Nairobi akaenda kumtia maneno maneno Neyo na kuvuruga mipango yote ya Ali na Neyo...mwisho wa siku Neyo akafanya Solo project na Diamond badala na Ali Kiba kama Neyo mwenyewe alivyotaka.

4.Show ya Chriss Brown,Monbasa

Juzi tena show sio yake haimuhusu ila alishinda Back stage kutoa figisu figisu...Ali alitakiwa afanye live show..na kufunga vifaa vya live show ingechukua zaidi ya Dakika 30 pale jukwaani alafu Ali ndio apande na hilo alikuwa tatizo la Ali bali ni la waandaaji wa show na fundi mitambo walichelewa kufunga mitambo yao.

Wizkid afanyi live show Anafanya semi live show ambayo Inawekwa CD yenye beat tupu na yeye anaimba juu yake.
Ali akamshauri kwa kuwa kufunga mitambo itachukua muda mrefu basi ni bora Wizkid apande afanye semi live show kwa maana mpaka Wizkid akimaliza show yake wale mafundi watakuwa washamaliza kazi yao na Ali atapanda kupiga Live show sasa kilichotokea Sallam akamwambia Meneja wa Wizkid Mr.Sande kuwa asikubali hapo ndio ulipotokea mzozo kati ya Ali na Team ya wizkid wakiongozwa na mfitini Sallam.

Mwisho wa siku walipoteza zaidi ya Dakika 40 yote kutaka kumkomoa Ali kwa kitu ambacho kipo wazi kabisa.

Mpaka Ali alipopanda muda ulikuwa ushapita na kupelekea kuzimiwa Mic na team ya Chris Brown kwa sababu ndege ulikuwa inawasubiri Airport kuwarudisha marekani.

Mwisho wa siku hakuna Bifu kati ya Ali na Naseeb ni washkaji ila kuna Beef kati ya Ali na Sallam.

Jozey The Boy inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Instagram na Twitter ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment

copyright © 2016 Jozey The Boy. Powered by Blogger.